THIS BLOG IS DESIGNED FOR INQUIRIES ABOUT HEALTH ISSUES OF CHILDREN. IT PROVIDES FAMILIES WITH PERSPECTIVE,ADVICE AND COMFORT ABOUT WIDE RANGE OF PHYSICAL,EMOTIONAL AND BEHAVOURAL ISSUES THAT AFFECT CHILDREN AND ADOLESCENTS. IF YOU ARE LOOKING FOR INFORMATION YOU CAN TRUST ABOUT YOUR CHILD KEEP ON VISITING US! THE BLOG ENCOMPASSES PANEL OF EXPERTS IN PAEDIATRICS AND CHILD HEALTH WITH EXTENSIVE KNOWLEDGE, AND ENSURE THE INFORMATION IS UP-TO-DATE.
Sunday, February 17, 2013
KUKOSA HAMU YA KULA KWA WATOTO!
kukosa hamu ya kula huwatokea watoto wengi hasa wale wenye umri kati ya miaka 2-6. Wazazi huwa na wasiwasi sana mtoto wao asipokula vizuri,lakini tatizo hili husababishwa na nini? kama mtoto hana ugonjwa wowote basi sababu huwa hii
- kwa kawaida mtoto anapofikisha umri huo huwa ukuaji wake (rate of growth) hupungua na mahitaji ya virutubisho vya mwili (nutrition requirements) pia hupungua.Wakati huu watoto huwa wanaanza kujifunza kujitegemea kwa kuanza kuchagua vile wanavyovipenda na vile wasivyovipenda.ni vizuri kutambua hii ni kawaida kwa watoto katika umri huu!
Wednesday, February 13, 2013
VIPELE VYA ALLERGY KWA WATOTO....UTAVIGUNDUAJE?
Kwa kawaida vipele vya allergy kwa watoto huwaanzia usoni au kwenye mikunjo ya mikono na magoti na mara nyingi huwa vinawasha na mtoto hujikuna sana.
Tuesday, February 5, 2013
UMUHIMU WA MAZIWA YA MAMA! UNASEMAJE
- Watoto wanaonyonya maziwa ya mama hupata kinga nzuri dhidi ya magonjwa mengi kama kisukari,kansa na magonjwa ya moyo.
- Maziwa ya mama humsaidia mtoto asipatwe na magonjwa ya kuhara.
- Humsaidia mtoto asipatwe na magonjwa ya meno kama kuoza.
Saturday, February 2, 2013
DAWA BARIDI NA MAFUA! WATOTO JE!
Wataalamu wanashauri kutotumia dawa baridi (over the counter) kutibu
magonjwa ya kikohozi na mafua kwa watoto wadogo. Tafiti zinaonesha
kwamba hazisaidii kupunguza dalili za ugonjwa kwa watoto wenye umri
mdogo. Na huweza kuwa sumu, hasa pale ambapo hutumika zaidi ya dose
iliyowekwa(over dose) .
MAFUA NA WATOTO! UFANYE NINI UKIWA NYUMBANI?
Mafua kwa watoto limekuwa tatizo linalowasumbua wakina mama wengi! unaweza kuanza kufanya yafuatayo ili kumsaidia mtoto!
- ana mafua mazito ambayo yanamkosesha kupumua vizuri
- mafua yanatoka mfululizo kama maji
- muweke mtoto apumzike sehemu yenye hewa ya kutosha na salama kama kitandani
- mpe fluids(maji,au juice ya matunda) kwa wingi hasa yenye Vitamin C
- anapokuwa na joto mpatie paracetamol (panadol) badala ya aspirin
- atahitaji uangalizi wa karibu au mpeleke kwa daktari kama kuna yafuatayo
- ana mafua mazito ambayo yanamkosesha kupumua vizuri
- mafua yanatoka mfululizo kama maji
Subscribe to:
Comments (Atom)




